KUFURU YA SINGIDA BLACK STARS KUZINDUA UWANJA HUU

 

Na Paschal D.Lucas (Mwanza)

Klabu ya Singida Black Stars imetangaza rasmi uzinduzi wa uwanja wao mpya wa kisasa unaoitwa Airtel Stadium, uliopo katika eneo la Mtipa, mkoani Singida.


Uzinduzi wa uwanja huo mpya wa klabu hiyo utafanyika Machi 24, 2025, mkoani Singida, ambapo watacheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Wananchi, Yanga SC.


"Airtel Stadium ni sehemu ya dhamira ya Singida Black Stars ya kuwekeza katika maendeleo ya michezo kwa kutoa mazingira bora kwa wachezaji, mashabiki, na jamii kwa ujumla. Uwanja huu umejengwa kwa viwango vya kimataifa na unatarajiwa kuwa kitovu cha mashindano makubwa ya kitaifa na kimataifa," imeeleza taarifa ya klabu hiyo.

Comments

Popular posts from this blog

BREAKING NEWS: MKURUGENZI WA TANESCO AFARIKI BUNDA KWA AJALI

MIAKA 30 JELA NGUNO WA KWIMBA KWA KUMBAKA KIZIWI

TANZANIA YAISHUKURU ITALIA KUHUSU SGR