BREAKING NEWS: MKURUGENZI WA TANESCO AFARIKI BUNDA KWA AJALI
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mhandisi Gissima Nyamo-Hanga amefariki dunia kwenye ajali ya gari iliyotokea wilayani Bunda Mkoa wa Mara.
Meneja wa TANESCO Mkoa wa Mara, Nickson Babu amethibitisha taarifa hizo ambapo amesema Nyamo-Hanga amefariki dunia pamoja na dereva wake.
Miili ya marehemu imehifadhiwa katika Hospitali Teule ya Wilaya ya Bunda.

Comments
Post a Comment