TANZANIA YAISHUKURU ITALIA KUHUSU SGR
Na Paschal D.Lucas
Serikali ya Tanzania kupitia Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, ameishukuru Italia kwa kutoa dhamana ya mkopo wa kujenga Reli ya Kisasa (SGR), kipande cha Kwanza na cha pili kuanzia Dar es Salaam, Morogoro, Dodoma hadi Makutupora, ambavyo ujenzi wake umekamilika na Treni kuanza kutoa huduma kuanzia Dar es Salaam hadi Dodoma.
Katika Picha hiyo ya hapo chini ni Waziri wa Fedha Mhe.Mwigulu Nchemba akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Italia (SACE) Bi. Alessandra Ricci, Mjini Rome Italia.

Comments
Post a Comment